Jumanne, 1 Agosti 2017

muendelezo wa MIRADI YENYE GHARAMA NDOGO YA UENDESHAJI LAKINI FAIDA KUBWA.


MRADI WA KUFYATUA TOFARI

Ukuaji wa mji unategemea sana Ukuaji wa sekta ya ujenzi, kila mmoja anawaza kujenga kama sio nyumba basi Itakuwa fensi kuzunguruka nyumba. Limekuwa hitaji la muhimu sana kwa wateja kupata tofari kwa haraka,  tofari imara na nzuri.  Kumbe ukiwa na mashine yenye uwezo mzuri na ukatengeneza Tofari lenye sifa wateja wanahitaji unaweza tajilika kwa kasi ya ajabu.

MASHINE YA KUFYATULIA TOFARI
Kwa sababu ya kasi ya uhitaji wa wateja, ni vyema kutumia mashine ya  kufyatua ya umeme,  ambayo itaendana na kasi ya uhitaji wa wateja.
Mashine hii ya umeme kwa siku nzima inauwezo wa kufyatua TOFARI 1300,
Hivyo kwa kuwa inahusika katika kazi ngumu sana lazima iwe imeundwa kwa vyuma imara  ili kuruhusu uzarishaji huo.

VITU VYA MUHIMU KUZINGATIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI HUU

1. RATIO YA CEMENT KWENYE UDONGO
Wengi huitaji faida kubwa hivyo kuweka uwiano mdogo kati ya cement na mchanga,  kupelekea biashara kuwa ngumu na kukaribisha sifa mbaya kwenye biashara hii,  hivyo kuwaharibia wale wanaotengeneza kiusahihi. Ratio nzuri na bora ni Tofari 40 kwenye mfuko au Tofari 45 kwa mfuko,  sasa unakuta mtu anatoa Tofari 50 kwenye mfuko kiasi kwamba mchanga na cement havishikani,  ukipitisha kidole kwa kukandamiza unatoka mchanga. Hii haifai.

2. MUDA WA KU VIBRATE NA KUKANDAMIZA MFUNIKO.
mashine hii ya umeme inakifaa maalum cha kushindilia udongo kwa kutetemesha hivyo sasa operator lazima atumie mda kidogo kutetemesha ili udongo ushikane Vinginevyo hautashikana na kupelekea kutoa Tofari lisilo imara. Pamoja na hilo lazima ukandamizaji wa mfuniko wa juu uendane na utetemeshaji wa Mashine.

3. MADINI YALIYOMO KWENYE MCHANGA  WA KUFYATULIA.
Kuna baadhi ya madini ambayo si rafiki na Cement, ata ukiweka ratio ya 10 lakini Tofari bado lingetoka sio imara,  hivyo ni muhimu kuchunguza content ya mchanga kabla haujaanza uzarishaji. Madini kama chumvi (NaCl) si rafiki na cement kabisa huzidisha unyevu na kupelekea cement kuishiwa nguvu yake kutokana na reaction kati yao.

4. UMWAGILIZIAJI WA MAJI MDA MCHACHE BAADA YA UFYATUAJI
Uimara wa Tofari lililozingatia vigezo vingine vyote hapo juu unategemea umwagiliaji wa maji.  Tofari imara linahitaji maji mengi baada ya kufyatuliwa.

BEI YA TOFARI
Wengi wanauza 1000/= lakini hawajawa wazi kwa ratio ipi?  Sasa kwa lengo la kuleta utofauti unaweza kufyatua TOFARI zenye ratio tofauti tofauti na bei ikawa tofauti. Mfano ratio ya 40 ukauza 1300/= na usafiri, 1200/= bila usafiri,  ratio ya 45 ukauza tsha 1100/= na usafiri, 1000/= bila usafiri.
Kumbe kwa uwezo wa kuzarisha Tofari 1300 kwa siku, utaingiza tsh 1,300,000/=, kwa idadi hii unauhakika wa kupata faida ya tsh 300,000/=.
Itaendelea wakati mwingine endelea kutufatilia ujue zaidi 

Maoni 1 :

  1. Hyo mashine ya umeme ya kufyatua tofali being gan

    JibuFuta

CHANGAMOTO WANAZOKABILIANA NAZO VIJANA KATIKA UANZISHAJI WA MIRADI NA SULUHISHO LAKE

Kwa mda mrefu changamoto ya vijana ni mtaji, na hata mwenye mtaji hajui nini afanye. Wengi imepelekea kuishia kumaliza mitaji yao...