Jumatano, 26 Julai 2017

MIRADI YENYE GHARAMA NDOGO YA UENDESHAJI LAKINI FAIDA KUBWA

    Watu wengi wenye pesa hushindwa au huwa na wakati mgumu katika kufikilia au kuanzisha miradi yenye faida kubwa,  ambapo hubaki kuigiliziana kupelekea wigo wa mapato kuwa mdogo sana kiasi cha kujihusisha na ushirikina wakizani ndio itakuwa njia sahihi ya kupambana na ushindani na kujipatia wateja wengi,  kitu ambacho huwa ni tofauti.

Katika biashara hasa unapotaka kuanzisha mradi mpya usifikili sana kitu kipya ambacho hakipo, kwani itawachukua mda mrefu wateja kuzoea na kuona umuhimu wa biashara hiyo kwao,  lakini pia ukifanikiwa wengine wenye pesa wataiga na kuanza kukuletea changamoto za ushindani.  na inauma sand pale unapojua wewe ndio muasisi wa fikra, labda ukisha fanikiwa uende ukaisajili COSOTA upate umiliki wa aidia yako na yoyote atakaeingia utamshtaki,  lakini nayo ni ghari sana, na inahitaji mda pia.
 
Cha msingi cha kufanya ni kubaki katika ile ile miradi ya zamani ambayo wengi wanafanya ila wewe utafute utofauti wake ili kuendana na ushindani.

MIRADI YENYE FAIDA KUBWA ZAIDI

1. MASHINE YA KUKOBOA NA KUSAGA UNGA.
Huu ni mradi maarufu sana na asilimia kubwa sana ya wenye pesa wanafanya mradi huu. Lakini kama nilivyokwisha sema hapo juu : ni vyema kujihusisha na miradi ambayo wengi wanafanya kuliko kuanzisha mradi mpya cha, msingi ni kuweka utofauti tu.
Mashine ya kusaga No.  35 inauzwa tsh 800,000/=,  kwa kuanzia unaweza kununua hii mashine kwanza ila badae ukikomaa kibiashara unaweza kununua mashine nyingine aina ya LB7 AU LB4  ambazo bei yake ina range kati Milioni moja na mbili,  ila uzalishaji wake unakuwa mkubwa zaidi ya NO. 35 au 50. Gharama za kuunganisha umeme ni tsh 400,000/=, mota moja inauzwa tsh  1200000/= mpaka 1500000/=

Unaweza toa huduma ya kusaga kwa wateja wadogo wadogo, ambayo ndio kawaida,  lakini pia ukasaga kwa ajili ya kufunga unga kwenye viroba na kuuza kwenye maduka ya jumla na rejareja pia, maana yake unakuwa na bland yako.
Bado pia pumba ni bidhaa adimu sana na inahitajika sana kwa wafugaji. Mikoa kama Tabora pumba inabei rahisi sana lakini mikoa kama Mwanza,  Arusha na Kilimanjaro pumba inabei sana,  usafirishaji kwa gunia ina range kwenye 3000/= mpaka 5000/=.

Bado pia mashine hizo hizo unaweza kusaga chakula cha kuku na ukakifunga kwa ujazo maalum, cha msingi sana kwenye chakula cha kuku ni kuakikisha unaweka content zote muhimu,  yaani virutubisho muhimu uakikishe vimo Vinginevyo wateja watakukimbia.
Mpaka hapo utakuwa tofauti na wengine wengi wenyekutoa huduma sawa na wewe.

SIFA YA KINU IMARA
1. Kinu imara kinatakiwa kuundwa kwa kutumia plain ion sheet yenye unene wa millimeter kuanzia 5 mpaka 8, ili kuepuka kutoboka au kwisha haraka
2. Feni kubwa kwa uwiano na size ya kinu ili kuharakisha usafirishaji wa unga toka kwenye kinu mpaka kwenye mfuko
3. Beseni kubwa linaloruhusu kuweka mzigo mwingi kwa wakati mmoja.

Itaendelea wakati mwingine endelea kutufatilia ujue zaidi juu ya miradi yenye faida kubwa zaidi.

Maoni 1 :

  1. Harrah's Reno Hotel & Casino - JT Hub
    Find 경산 출장안마 out the hours, maps, 보령 출장샵 phone numbers, hours, 경기도 출장샵 directions, and more for Harrah's Reno Hotel & Casino - 777 Harrah's Rincon Way, 충청남도 출장샵 Reno, NV 김천 출장안마 89449.

    JibuFuta

CHANGAMOTO WANAZOKABILIANA NAZO VIJANA KATIKA UANZISHAJI WA MIRADI NA SULUHISHO LAKE

Kwa mda mrefu changamoto ya vijana ni mtaji, na hata mwenye mtaji hajui nini afanye. Wengi imepelekea kuishia kumaliza mitaji yao...