Jumatano, 28 Agosti 2024

CHANGAMOTO WANAZOKABILIANA NAZO VIJANA KATIKA UANZISHAJI WA MIRADI NA SULUHISHO LAKE

Kwa mda mrefu changamoto ya vijana ni mtaji, na hata mwenye mtaji hajui nini afanye. Wengi imepelekea kuishia kumaliza mitaji yao na kurudi vijiweni. Imedhaniwa na vijana wengi kwa sababu ya kukosa miongozo au washauri au watu wa kuwashika mikono katika njia zao za mafanikio kuwa kuuza nguo, au viatu au cd, au wigi za wakina mama na nyingine za kufanana na hizo ndo kazi zenye pesa. Mwisho wa siku matokeo huwa tofauti na nguo kujaa vumbi, maana wauzaji wamekuwa wengi. Katika haya maisha cha msingi sana ili kupata pesa na mafanikio yoyote, 1. Ujulikane mpaka watu waku- rebel. Vijana rudia kuisoma hii point uielewe vyema. Kwenye ishu yoyote unatakiwa kukomaa, kung'ang'ania kiasi cha kuhakikisha unajulikana kwa lile unalolifanya. Hili sio zoezi la siku au miezi, hili ni zoezi la mwaka au miaka wakati mwingine. Sio leo unauza cd, kesho unauza soda. 2. Fanya tofauti. Kila ulifanyalo fanya tofauti na namna jamii imezoea au wengine wafanyavyo. Kama unauza mchele, mfungashie na chumvi kijiko kimoja. Watu hawatanunua mchele mtupu na wakwako una chumvi 3. Usiiache biashara yako ijiendeshe. Usiwe mfanyabiashara wa kungoja mteja, pambana kwa mbinu mbalimbali kumvuta mteja, toka nje ya duka kumfata mteja, mbinuka, mjulie hali mteja wako mkubwa akikosekana siku moja, toa huduma ya kuwapelekea wateja bidhaa nyumbani. Pamoja na mbinu izo biashara ya maduka imekuwa kubwa kila kona maduka yamejaa, kwanini usifikilie kuanzisha viwanda vidogo vidogo, ambapo wengi bado hawajawazia, miongoni mwa viwanda vidogo vidogo ni pamoja na:- 1. Mashine za kusaga peanut butter. Hii haiitaji mtaji mkubwa sana kuanza. Ili kiwanda kidogo kikamilike, kunahitajika uwe na mashine ya kukaanga, mashine ya kukoboa karanga zilizokaangwa na mashine ya kusaga karanga. Kiasi cha tsh 4,500,000/= kina tosha kupata mashine zote. Hii biashara inahitajika kufanywa kwanza kwa kutoa huduma kwa wateja wa kila siku wanaosaga kilo 1, 5, 10...nk, lakini pili kwa kusaga karanga zako mwenyewe kwa ajili ya kufungasha ( packing ). Wateja ni shule za kindergarten, shule za boarding, supermarkets, masoko makuu na wateja wadogo wadogo. MASHINE YA KUSAGA PEANUT BUTTER YA UMEME
Hizi ni mashine zinazotumia umeme wa nyumbani yaani single phase. Mashine ya kusaga karanga inasaga mpaka kilo 24 kwa unit moja ya umeme. Ambapo tanesco wanauza unit tsh 400, mfano ukisaga kilo tsh 200 inamaana utapata tsh 4800 kwa unit, faida 4400, ukisagia kilo tsh 300 utapata 7200 faida 6800/= kwa unit.
Ili kuharakisha na kuendana na ukuaji wa soko utatakiwa uwe na mashine ya kukoboa, (picha yake apo juu) hii hutoa vile viganda laini baada ya kukaangwa. Mashine nyingine yenye umuhimu sana ni mashine ya kukaanga. Gharama kwa mashine moja moja kuinunua ni kama ifuatavyo:- 1. YA KUSAGA 1,500,000/= 2. YA KUKOBOA NA KUPETA TSH 1,500,000/= 3. YA KUKAANGA KILO 10 TSH 1,500,000/= JUMLA TSH 4,500,000/= Watengenezaji wazuri wa mashine izo ni T.G.M DESIGNER, Ni kiwanda kidogo sana jiji mwanza ila wanaumakini mkubwa katika kutengeneza mashine bora na imara, wanaushauri mzuri pia na wana guarantee, kwa kipindi flani mashine inakuwa chini yao. Kitu ambacho hauwezi pata toka viwanda vingine. Wanajua capacity ya mota inayohitajika kwa kila mashine Wanatarajia kuanzisha mradi darasa ambapo wateja wao watakaribishwa kujifunza na kuona wigo wa faida, changamoto na namna ya kukabiliana nazo. Tembelea @tumbo51 tiktok, T.G.M designer Facebook, tumbokabona Instagram, T.G.M designer WhatsApp Unaweza wasiliana nao kwa sim 0683628498 au 0679128498 ..........itaendelea part two kiwanda kidogo tofauti ambacho hautajutia kuwa nacho

Jumapili, 26 Februari 2023

MASHINE BORA ZA KUSAGA KARANGA KUWA PEANUT BUTTER ZA UMEME

inatumia umeme wa nyumbani, kwa siku inasaga mpaka gunia 6 za karanga zilizokaangwa vizur. kama unatoa huduma kwa jamii, na ukawa unasaga kilo moja kwa 300/= unit moja itakupatia tsh 8000 wakati unit moja tanesco wanauza tsh 300, hivyo utapata faida ya tsh 7700. kwa mawasiliano piga sim 0683628498

Jumanne, 21 Februari 2023

MASHINE YA KUKOBOA KARANGA ZILIZOKAANGWA

Ni mashine inayotumia umeme wa Nyumbani, inakoboa karanga zilizokaangwa kwa ajili ya kusagwa kuwa peanut butter. Ni mashine inatengenezwa na kiwanda cha Tumbo Makufuli Workshop na T.G.M designer, kwa mawasiliano piga sim 0683628498 au kwa email: tumbokabona@gmail.com

Ijumaa, 23 Agosti 2019

UBORA WA JUICE YA MIWA

Inafurahisha kuona kuwa wapo wafanyabiashara wengi maeneo tofauti tofauti Nchini mwetu na mitaa tofauti tofauti wanaouza juisi ya miwa.
Kimsingi juisi hii ni sukari halisia ambayo haijachakatwa.​
Sukari halisia ni nzuri kwa mwili kwani ina virutubisho na madini kwa wingi.



Miwa ina faida nyingi kiafya. Juisi ya miwa inafahamika na wataalamu wa afya kwa kuwa na uwezo wa kuupa mwili nguvu kwa sababu ya ‘glucose’ iliyopo.
Kijiko kimoja cha juisi ya miwa, kina kalori 11. Madini halisi na vitamin zinazopatikana katika sukari ni kama phosphorus, calcium, madini ya chuma na potassium.



Si hivyo tu, miwa ni jamii ya tunda lenye alkali hivyo lina uwezo wa kupambana na saratani hasa ile ya kibofu cha mkojo na saratani ya maziwa.
Miwa ina upekee wake kwani ina uwezo wa kuongeza maji mwilini, inaupooza mwili na kuupa nguvu.


Virutubisho vilivyopo katika miwa vina manufaa makubwa katika kusaidia utendaji kazi wa ogani muhimu kama figo, moyo, ubongo na viungo vya uzazi.
Pia, wagonjwa wa kisukari wasihofie sukari iliyopo kwenye miwa kwani haina madhara yoyote kwao. Uzuri wa juisi ya miwa ni kuwa sukari yake ni halisia.​

Mradi wa ukamuaji juice ya miwa ni mradi ambao unakipato kizuri sana kwani miwa ni mingi sana Tanzania kiasi cha kuweza kupata super profit. Lakin pia watu wamepata elimu na kuwa na muamko sana katika kuweka miili yao katika ubora
Mashine nzur ni.zile ambazo zitatengenezwa kwa kuzingatia afya na usafi wa mashine. Watengenezaji wazuri.wanaozingatia ubora ni T.G.M designer ya mwanza 0683628498. Na T.M.W ya tabora.

kwa wahitaji wa mashine bora na imara kabisa sasa wanaweza wasiliana na hawa T.G.M DESIGNER NA T.M.W

Jumanne, 4 Desemba 2018

UTAMBULISHO WA TAWI JIPYA MWANZA

T.G.M DESIGNER ni kifupi cha Tumbo General Machine Designer. Hili ni jina la kiwanda au tawi jipya la kiwanda mwanza. Baada ya kiwanda mama Tabora kinachoitwa T.M.W yaani Tumbo Makufuli Workshop sasa kimezaa tawi mwanza T.G.M Designer. Kiwanda kinapatikana ilemela karibu na PP HOTEL. Tunajihusisha na kazi zote kama zinazofanywa na kiwanda mama Tabora

NEMBO

Slogan yetu ni " your life simplified with our makes" yaani maisha yako yanarahisishwa na tunavyounda. Na ili yarahisishe lazima uwe tayali kama mteja kututyma kazi. Na ili ututume lazima tuwe wakweli, wapole, wastaarabu, wanyenyekevu na ubora wa kazi zetu. Na haya ndio malengo na maisha tuliyochagua na wateja wetu. Kwa chochote ambacho utahudumiwa visivyo usisite kuwasiliana nasi nakusema wazi. Maana amna mkamilifu duniani.

NEMBO KWA KIWANDA CHA TABORA

Jumapili, 28 Januari 2018

UTARATIBU MPYA WA UUZAJI BIDHAA ZETU KWA WATEJA WA MBALI

Tumekuwa na matangazo mengi online juu ya bidhaa zetu, matangazo tumeweka what'sapp, facebook, twitter, instagram, zoomtanzania, kupatana, na, tumbomakufuli.blogspot.com, sasa tumekuwa na wateja wengi online kuliko wanaotufikia kiwandani kwetu. Hii inaleta haja ya kuboresha njia ya biashara kimtandao  kuifanya bora na salama kwa mteja na kwetu pia.
tunajinsi mbili za kufanya biashara hii ni uchaguzi wako mteja juu ya njia ipi utaona salama kupata bidhaa yako.

NJIA YA KWANZA
Ukipendezwa na bidhaa yetu kwanza waasiliana nasi kujua kama ipo, na kutoa vigezo ambavyo wewe unahitaji, vikiwiana na ukawa na utayali wa kununua, nenda kwenye ofisi za usafirishaji unazozijua na kuziamini kama ni mabasi au image power, wakuunganishe na wakala wao au ofisi yao iliyopo tulipo sisi kama kiwanda. kwa sasa tupo mwanza kama branch, na target market. ingawa makao makuu yapo Tabora lakini bidhaa zote huletwa mwanza kwa mauzo. kwa iyo watakuunganisha na wakala wa mwanza, utampa vigezo unavyotaka vya bidhaa husika. mimi ntapeleka bidhaa hiyo kwa wakala au ofisi ya usafirishaji utanipa jina la huyo uliemuomba ubalozi, ntamuonyesha tutatest mbele yake akilidhika atakukikishia kuwaa kila kitu kipo sawa na wewe utanitumia pesa ya kununulia bidhaa hiyo ntaiacha hiyo biddhaa hapo ofisini kwa usafirishwaji

NJIA YA PILI
Hii inapendeza kwa wateja ambao tulishafanya biashara mara ya kwanza au atakama anaanza biashara na sisi kwa mara ya kwanza ila amepewa ushuhuda kwa mteja wetu ambaye tulishafanya biashara nae
ambapo mteja ataulizia bidhaa aitakayo kama ipo, na kama ipo atatakiwa kutuma hela moja kwa moja kwangu na hatua zaidi zitafuata

Nje ya taratibu hizi TUMBO MAKUFULI WORKSHOP haitajiingi kwenye biashara yoyote na wateja wa mbali au wamitandaoni

ASANTENI NA KARIBUNI SANA

Jumatatu, 21 Agosti 2017

muendelezo : MRADI WA KUSAGA KARANGA KUWA NTWILI


MRADI WA MASHINE YA KUSAGA KARANGA KUWA NTWILI
Katika historia ya usagaji karanga, wazee wetu kwenye karne ya kumi na tisa walikuwa wanasaga kwenye mawe. Ambapo kunajiwe kubwa na dogo ambalo ndo anapitisha juu ya karanga ambazo zinakuwa kati ya jiwe dogo na kubwa na kusugua kwa mikono miwili.
Baadae waliboresha wakatengeneza ubao unaoitwa mbehe na msiginio hivi Vilikuwa vya mbao,  lakini bado ufanisi ulitosheleza maisha ya kipindi chao.  Kwa sasa kumekuwa na gunduzi mbalimbali za Mashine za kusagia karanga ambazo zimekuwa ni bora kuliko hizo nilizoeleza hapo juu. Zimeundwa kwa chuma husaga kwa uharaka zaidi. Zipo za mkono



Na zipo za umeme, ila hizi za umeme ni maalum kwa biashara,   yaani unasaga ili uuze karanga Kama bidhaa.

KWA NINI USAGAJI WA KARANGA NAO UMEKUWA MRADI
usagaji  wa Karanga Umekuwa mradi kutokana na sababu nyingi sana;
1. Wingi wa majukumu kwa wahitaji. Wahitaji wengi wa karanga iliyosagwa wanabanwa na majukumu aidha ya kiofisi au ata ya nyumbani kiasi kwamba kupata mda wa kusaga karanga kwa matumizi yake anaona uzito. Hivyo kutoa nafasi kwa wengine kuuza madukani hizi karanga.
2. Upatikanaji wa karanga sehemu flani kuliko sehemu nyingine; mfano Tabora inasifika sana kwa Karanga hasa wilaya ya urambo, lakini Arusha ni adimu, hivyo wenyekuzijua fulsa wanasaga Karanga nakuzisafirisha mikoa ambayo kunauadimu.
3. Uhitaji wa utofauti kati ya mtu na mtu katika kuanzisha miradi. Ile hali ya kutaka kuwa tofauti kati ya wadau, huchochea mtu kufikilia zaidi na kufikia katika kuanzisha miradi ambayo huwa na Matokeo mazuri. Na hapo watu wakaanzisha mashine hizi ili kuwa tofauti.

NAMNA YA UENDESHAJI WA MRADI WA USAGAJI WA KARANGA.
Kwanza ni lazima ulijue soko lako. Na liwe la uhakika, hii ujulikana kwa kufanya tafiti za soko (marketing research). Ukijua lilipo soko jua unahitajika kuandaa bidhaa yako.

Kutegemea na kiwango cha uhitaji wa wateja wako, unaweza anza na mashine za mkono ambazo nikubwa. Zinauzwa tsh 80,000/=. Ambapo mtengenezaji na msambazaji mkubwa ni Tumbo Makufuli Workshop wa Tabora. Ambao unaweza kuwapata kwa simu no +255683628498, unaweza nunua mashine mbili za mikino ili uendane na wateja wako.

Kama uhitaji ni mkubwa Sana,  unaweza nunua mashine ya kusaga karanga ya umeme . Pia Mafundi na wasambazaji ni haohao Tumbo Makufuli Workshop. Bei ya mashine hii ni tsh 1000,000/= inauwezo wa kusaga gunia moja na nusu kwa siku. Sasa kwa hii mashine unakuwa na kiwanda kamili.

Baada ya usagaji Unatakiwa kuwa na vifungashio vyenye muonekano mzuri na safi. Hii itakufanya uweze kuuza mpaka kwenye supermarkets mbalimbali. Package nzuri na brand name yako pia itakupa umaarufu.

Pia katika misingi ile ile ya kuleta utofauti, Kama mtakumbuka huko nyuma tulizungumzia hili,   unaweza kuzarisha bidhaa zote zitokanazo na Karanga,  mfano mafuta ya karanga, pinnate butter , mashudu ya Karanga kwa ajili ya mifugo. Karanga za kutafuna za kawaida na za mayai. Kwa hili lazima uwe na duka kamili kwa bidhaa zako tu,  uwe na brand yako ambayo inazingatia ubora na viwango.

WAPI WATEJA WANAPATIKANA
soko la Karanga ni kubwa sana, kwa hapa kwetu jamii nyingi zimekuwa zinatumia Karanga kama kiungo kwenye mboga au chakula cha watoto,  pia karanga zimechukua nafasi ya Jojo tangu pale zilipogundulika athari za Jojo mwilini  mwetu.  Hivyo ata eneo ulipo wateja wapo.
Lakini pia nchi jirani kama Malawi wanauhitaji mkubwa wa hii bidhaa ya karanga.
Lakini Kama haitoshi,  kuna mikoa ambayo inauhaba wa karanga kutokana na ukweli kwamba wao hawalimi karanga,  napo nisehemu muhimu kupeleka bidhaa hii.

Itaendelea tena wakati mwingine. Usisite kutoa maoni yako na kujiunga nasi ili uweze kupata mwanga na baadae kuwa na uhakika wa nini cha kufanya

Jumanne, 1 Agosti 2017

muendelezo wa MIRADI YENYE GHARAMA NDOGO YA UENDESHAJI LAKINI FAIDA KUBWA.


MRADI WA KUFYATUA TOFARI

Ukuaji wa mji unategemea sana Ukuaji wa sekta ya ujenzi, kila mmoja anawaza kujenga kama sio nyumba basi Itakuwa fensi kuzunguruka nyumba. Limekuwa hitaji la muhimu sana kwa wateja kupata tofari kwa haraka,  tofari imara na nzuri.  Kumbe ukiwa na mashine yenye uwezo mzuri na ukatengeneza Tofari lenye sifa wateja wanahitaji unaweza tajilika kwa kasi ya ajabu.

MASHINE YA KUFYATULIA TOFARI
Kwa sababu ya kasi ya uhitaji wa wateja, ni vyema kutumia mashine ya  kufyatua ya umeme,  ambayo itaendana na kasi ya uhitaji wa wateja.
Mashine hii ya umeme kwa siku nzima inauwezo wa kufyatua TOFARI 1300,
Hivyo kwa kuwa inahusika katika kazi ngumu sana lazima iwe imeundwa kwa vyuma imara  ili kuruhusu uzarishaji huo.

VITU VYA MUHIMU KUZINGATIA KATIKA UTEKELEZAJI WA MRADI HUU

1. RATIO YA CEMENT KWENYE UDONGO
Wengi huitaji faida kubwa hivyo kuweka uwiano mdogo kati ya cement na mchanga,  kupelekea biashara kuwa ngumu na kukaribisha sifa mbaya kwenye biashara hii,  hivyo kuwaharibia wale wanaotengeneza kiusahihi. Ratio nzuri na bora ni Tofari 40 kwenye mfuko au Tofari 45 kwa mfuko,  sasa unakuta mtu anatoa Tofari 50 kwenye mfuko kiasi kwamba mchanga na cement havishikani,  ukipitisha kidole kwa kukandamiza unatoka mchanga. Hii haifai.

2. MUDA WA KU VIBRATE NA KUKANDAMIZA MFUNIKO.
mashine hii ya umeme inakifaa maalum cha kushindilia udongo kwa kutetemesha hivyo sasa operator lazima atumie mda kidogo kutetemesha ili udongo ushikane Vinginevyo hautashikana na kupelekea kutoa Tofari lisilo imara. Pamoja na hilo lazima ukandamizaji wa mfuniko wa juu uendane na utetemeshaji wa Mashine.

3. MADINI YALIYOMO KWENYE MCHANGA  WA KUFYATULIA.
Kuna baadhi ya madini ambayo si rafiki na Cement, ata ukiweka ratio ya 10 lakini Tofari bado lingetoka sio imara,  hivyo ni muhimu kuchunguza content ya mchanga kabla haujaanza uzarishaji. Madini kama chumvi (NaCl) si rafiki na cement kabisa huzidisha unyevu na kupelekea cement kuishiwa nguvu yake kutokana na reaction kati yao.

4. UMWAGILIZIAJI WA MAJI MDA MCHACHE BAADA YA UFYATUAJI
Uimara wa Tofari lililozingatia vigezo vingine vyote hapo juu unategemea umwagiliaji wa maji.  Tofari imara linahitaji maji mengi baada ya kufyatuliwa.

BEI YA TOFARI
Wengi wanauza 1000/= lakini hawajawa wazi kwa ratio ipi?  Sasa kwa lengo la kuleta utofauti unaweza kufyatua TOFARI zenye ratio tofauti tofauti na bei ikawa tofauti. Mfano ratio ya 40 ukauza 1300/= na usafiri, 1200/= bila usafiri,  ratio ya 45 ukauza tsha 1100/= na usafiri, 1000/= bila usafiri.
Kumbe kwa uwezo wa kuzarisha Tofari 1300 kwa siku, utaingiza tsh 1,300,000/=, kwa idadi hii unauhakika wa kupata faida ya tsh 300,000/=.
Itaendelea wakati mwingine endelea kutufatilia ujue zaidi 

Jumatano, 26 Julai 2017

muendelezo: MIRADI YENYE GHARAMA NDOGO YA UENDESHAJI LAKINI FAIDA KUBWA.

Kipindi kilichopita tuliishia kwenye mradi wa Mashine ya kusaga na kukoboa nafaka. Ambapo leo tunaendelea na mapato inayoweza kupata kwa siku, pamoja na kujadili miradi mingine. Karibu.

MAPATO KWA SIKU
Kama unatoa huduma kwa wakazi wa jirani na mashine tu,  kusaga na kukoboa kwa siku unaweza ingiza kati ya tsh 90000/= mpaka 100000/= eneo ulipoweka mashine kuna population kubwa

Kama unatoa huduma kwa wakazi wa jirani na mashine pamoja na kusaga unga wa kufunga kwenye viroba kwa siku  unaweza ingiza kati ya tsh laki moja na nusu mpaka tatu.

WAPI UNAWEZA PATA MASHINE HIZI KWA HARAKA
Kwa sasa viwanda vingi vinatengeneza mashine hizi,  hivyo unaweza pata kokote kwa hapa Tanzania,  ila unapohitaji Mashine bora na imara ambayo itafikia vigezo tulivyotaja hapo juu, ni TUMBO MAKUFULI WORKSHOP pekee ambao wamebaki na sifa ya Kutengeneza bidhaa bora na imara. Wanapatikana Tabora Mjini,  kwa namba +255683628498 au +255757027691 au email: tumbokabona@gmail.com

2. MRADI WA KUCHANA MBAO KWA BENSAW
Bensaw ni mashine ya kuchana mbao yenye msumeno mwembamba uliopinda,  ni tofauti na mashine ya kuchana kwa msumeno wa duara.
Add BENSAW MACHINE. 


TOFAUTI KATI YA BENSAW NA MASHINE ZINGINE ZA KUCHANA MBAO
Bensaw inauwezo wa kuchana gogo lenye mduara wa kipenyo cha mpaka futi 2 au inch 24 wakati mashine zingine zinaweza kuchana gogo lenye mduara wa kipenyo cha mpaka futi 0.5 au inch 6 ambapo gogo mpaka ligeuzwe ili kutoa ubao au banzi lenye upana wa inch 12,  wakati mwingine njia hukosana, yaani ulipopita msumeno wa chini unakosana na utakaopita juu ili utoe banzi au ubao, hivyo kuacha kazi chafu isiyofurahisha Mteja

Tofauti nyingine ni muda wa utendaji,  kwa bensaw huchukua muda mfupi sana kutimiza kazi ambayo  mashine zingine zingefanya kwa muda wa mpaka mara tatu au nne ya muda huo

Bensaw huacha kazi safi sana ukilinganisha na mashine zingine

MAPATO YA SIKU YA BENSAW
Kwa siku unaweza ingiza kati ya tsh 100,000/= mpaka 200,000/= cha msingi ni kuweka Mashine kwenye maeneo ambayo kuna wakulima wa miti au mapori makubwa,  mfano unaweza kuweka Tabora Mjini au Mwanza,  sengelema, au mpanda.

NAMNA YA KULETA UTOFAUTI
Pamoja na huduma ya kuchana mbao kwa wateja wako,  unaweza kuanzisha unit yako inayoenda polini kuleta magogo wakati huo pia unanunua toka kwa watu baki kisha unachana mbao na Kusafirisha mikoani kama Dar-es-salaam au Mwanza.

Bado pia ukaweka unit nyingine ya Mafundi ambao wanatengeneza fenicha mbalimbali, kama kabati za kisasa, meza na viti pamoja na top za milango yenye muonekano wa kisasa na Kusafirisha kwenye miji mikubwa.

Pia maranda yanayotokana na uchanaji wa mbao unaweza tengeneza nishati mbadala ya kupikia badala ya kuyatupa,  na hivyo kujiongezea kipato

MAMBO YA KUZINGATIA KWENYE MRADI HUU

1. kuwa na vibari vya kuvuna maliasili kama hizo mbao. Vinginevyo utaiona chungu na haifai
2. Kwa kuanzia unaweza kufanya bila kulipa mapato TRA kwa kuwa unaanza, ila biashara  ikishamili lazima uakikishe kaisali anapata fungu lake.
3. Kutafuta eneo kubwa la kufanyia kazi,  maana wateja watakuja na magari yao yamepakia magogo, lazima eneo la kuweka magogo yao liwe kubwa na salama

BEI YA MASHINE YA BENSAW
mashine ya bensaw kwa sasa original inauzwa mpaka Milioni tisa bila mota. Inakuwa katika material ya dongo ambayo sikushauri kuwa na mashine yenye material haya kwani ni rahisi kuvunjika.
Tumbo MAKUFULI workshop wanatengeneza Mashine hiyohiyo kwa material ya chuma kwa tsh 6,500,000/=.



Itaendelea wakati mwingine endelea kutufatilia ujue zaidi, usisahau kutufollow apo chini na kuacha comment yako.  

WRONG WAY FOR INDUSTRIAL CHANGE IN AFRICA

Wrong way always end up  to wrong destinations, that may result to culture shock, this is what Africa industrialization process reach.
Changes to be effective should be gradual, this to give room for adapting it, and giving yourself chance to fix some of challenges which are always accompanied with changes to fit your life style, but also to evaluate the benefit of changes to your society. There are many reasons to why changes should be gradual, but my focus to write this is to spark the view on wrong way that Africa choose toward industrialization.

The history of industrialization is clear, industrialization was spearheaded with innovations and discovery, whereas small scale discoveries were change to large beneficial projects. The spirit of innovation and discovery is discouraged in Africa this is clear via a couple of examples, in Africa if a person discover a gun for example will be considered as wrong doer and strong measures will be taken upon him or her by the government.  In Mbeya region, in Tanzania there was a youth who was able to make an aeroplane, but the government was deef and brind on that,  till the external countries saw him and take him for training purposes.

When you hear about industrial change in African countries, we are focusing on initiate industries 99% with technology from abroad. Local industries are not know,  they seem as doing their day to day activities for subsistence only.

Wonderful enough, is that African governments are calm on success of internal industrial,  but external countries are fighting hard to take us from one stage to another of development, it is now wise for associations which focus to develop African local industries to go direct to those local industries otherwise  they would encounter some middlemen who may interrupt the benefits which are intended to local industries in a way that it may reach reduced or nothing.

Will continue soon.

CHANGAMOTO WANAZOKABILIANA NAZO VIJANA KATIKA UANZISHAJI WA MIRADI NA SULUHISHO LAKE

Kwa mda mrefu changamoto ya vijana ni mtaji, na hata mwenye mtaji hajui nini afanye. Wengi imepelekea kuishia kumaliza mitaji yao...