Jumamosi, 15 Julai 2017

UMUHIMU WA VIWANDA VIDOGO VIDOGO KATIKA MAISHA YA KILA SIKU.

Viwanda Vidogo Vidogo vimekuwa chachu ya maendeleo ya mtu mmoja mmoja na ata taifa kwa ujumla,  Ingawa mchango wake kwa taifa haujatiliwa maanani

Ni viwanda ambavyo Kimsingi ni kama mayatima  havina mlezi mwenye uhitaji wa Kweli wa kuwatoa, yaani kuwafanikishia matakwa yao hasa ya kukuwa na ata kuwa viwanda vya kati. Waliopo they act as middle man kutafuta kazi kwa jina la flani na kufanya wao kwa mafundi wao kwa manufaa yao. Ufatiliaji wa siku hadi siku wa maendeleo ya viwanda hivyo Kama hamna, wao wanangoja maonyesho na siku kaja mfadhili flani ndo uyawaona na matai na note book kwenye kila kiwanda ata kile cha uchocholoni. Hatutafika hivi. Imebaki juhudi ya fundi mwenye kiwanda kufikia hayo.

MCHANGO WA VIWANDA VIDOGO KATIKA MAENDELEO YA TAIFA
1. Viwanda hivi vinatoa ajila kwa vijana . Ajila inayotolewa ingawa ni ndogo ila inamaslahi makubwa sana katika ustawi wa taifa letu,  vijana ambao labda kwa kukosa cha kufanya wangeweza kuwa wavuta bangi, wizi, ubakaji na mengine mengi ya kufanana na hayo, sasa wanapata kazi ambayo inawaepusha na hayo kwani watakuwa bize na majukumu ya siku kiwandani

2. Upatikanaji wa bidhaa zinazofikia uhitaji wa wateja, viwanda Vidogo Vidogo mara nyingi hujihusisha na utengenezaji wa mashine ndogo ndogo ambazo huwa na ubora na uimara zaidi ya zile zitokazo nje, kwa vyuma ambavyohutumika ni imara na vizito kuliko, hivyo kukidhi haja ya wateja.

3. Kupunguza usumbufu wa kuagiza nje,  viwanda hivi hiweza kubuni Mashine mbalimbali kulingana na uhitaji wa Mteja, tu kwa kuwa wateja wengi hawajajua namna ya kuwatumia hawa Mafundi hapa ndo msukumo wa ubunifu unafia

4. vinasaidia katika mzunguruko wa mitaji.  Hii ni kwa mantiki moja, Fundi akinunua malighafi kwa ajili ya kazi zake ndio wanafanya existence ya maduka haya ya hardware , na ndio mitaji ya hao wenye maduka inakuwa na mzunguruko kufana, ata T. R. A wakizungurukia wanapata pato la taifa, hivyo uchumi wa taifa kukuwa.
Kwa leo tuishie hapo kwa yoyote mwenye Mawazo,  ushauri basi unakaribishwa


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

CHANGAMOTO WANAZOKABILIANA NAZO VIJANA KATIKA UANZISHAJI WA MIRADI NA SULUHISHO LAKE

Kwa mda mrefu changamoto ya vijana ni mtaji, na hata mwenye mtaji hajui nini afanye. Wengi imepelekea kuishia kumaliza mitaji yao...